MAONESHO YA WIKI YA UBUNIFU TANZANIA 2023
Chuo Kikuu cha Dodoma kinashiriki Maonesho ya Wiki ya Ubunifu Tanzania 2023, maonesho haya yanafanyika Uwanja wa Jamhuri- Dodoma
Karibu Banda la UDOM uone bunifu mbalimbali zilizofanywa na wanafunzi pamoja na wanataaluma mahiri toka UDOM, pia huduma mbalimbali kwa jamii zinatolewa kama kutengeneza simu, Kompyuta, Ushauri juu ya kutunza Kompyuta, Simu n.k huduma za vipimo kama kupima VVU/Ukimwi, Presha, uzito
NB: huduma zote zinatolewa bure