UJENZI WA KAMPASI YA NJOMBE UDOM WAANZA KWA KASI


  • 6 hours
  • The University of Dodoma

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Profesa Lughano Kusiluka, leo Septemba 9, 2025, ametembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Kampasi ya UDOM mkoani Njombe.

Profesa Kusiluka amesema ameridhishwa na hatua zilizofikiwa, lakini akamtaka mkandarasi kuongeza kasi ya ujenzi ili majengo yakamilike ifikapo Mei 2026, kama ilivyopangwa bila kuongeza muda.

Mshauri Elekezi wa Mradi, Mhandisi Filbert Shayo, amesema ujenzi umefikia asilimia 15 na hatua za msingi zinaendelea kukamilishwa.

Kampasi hiyo inatarajiwa kuwa chachu ya kuboresha elimu ya juu na kuchochea maendeleo ya kiuchumi nchini.

Comments
Send a Comment